1. SURAT AL-FAATIH'A
(Imeteremka
Makka)
Sura
hii iliteremka Makka kabla ya Hijra, kuhamia Mtume s.a.w. Madina. Imeitwa
Al-Faatih'a, yaani Kifungulio kwa kuwa ndiyo sura ya mwanzo katika mpango wa
Msahafu Mtukufu, nayo ni sura ya mwanzo iliyo teremka kwa utimilivu wake. Na
sura hii inakusanya jumla ya yaliyomo katika Qur'ani na kama kwamba huu ni
mukhtasari wake, na baadaye yatakuja mambo kwa tafsili, babu-babu.
Na makusudio ya Qur'ani ni: Kubainisha Tawhid, Upweke wa Mwenyezi Mungu; na
kubainisha ahadi na bishara kwa Muumini mtenda mema; na kubainisha ahadi na
onyo kwa kafiri na mtenda maovu; na kubainisha ibada; na kubainisha njia ya
kufanikiwa duniani na Akhera; na hadithi za walio mt'ii Mwenyezi Mungu
wakafuzu, na hadithi za walio muasi wakaangamia.
Sura Al-Faatih'a inakusanya kwa ufupi na kwa kuashiria makusudio haya, na kwa
hivyo ndio ikaitwa pia "Ummul Kitaab" yaani "Msingi wa
Kitabu".
1. KWA
JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.
2. Sifa
njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;
3. Mwingi wa
Rehema Mwenye Kurehemu;
4. Mwenye
Kumiliki Siku ya Malipo.
5. Wewe tu
tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.
6. Tuongoe njia
iliyo nyooka,
7. Njia ya ulio
waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.
|