Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 1. SURAT AL-FAATIH'A
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

1. SURAT AL-FAATIH'A

(Imeteremka Makka)

Sura hii iliteremka Makka kabla ya Hijra, kuhamia Mtume s.a.w. Madina. Imeitwa Al-Faatih'a, yaani Kifungulio kwa kuwa ndiyo sura ya mwanzo katika mpango wa Msahafu Mtukufu, nayo ni sura ya mwanzo iliyo teremka kwa utimilivu wake. Na sura hii inakusanya jumla ya yaliyomo katika Qur'ani na kama kwamba huu ni mukhtasari wake, na baadaye yatakuja mambo kwa tafsili, babu-babu.
Na makusudio ya Qur'ani ni: Kubainisha Tawhid, Upweke wa Mwenyezi Mungu; na kubainisha ahadi na bishara kwa Muumini mtenda mema; na kubainisha ahadi na onyo kwa kafiri na mtenda maovu; na kubainisha ibada; na kubainisha njia ya kufanikiwa duniani na Akhera; na hadithi za walio mt'ii Mwenyezi Mungu wakafuzu, na hadithi za walio muasi wakaangamia.
Sura Al-Faatih'a inakusanya kwa ufupi na kwa kuashiria makusudio haya, na kwa hivyo ndio ikaitwa pia "Ummul Kitaab" yaani "Msingi wa Kitabu".

1. KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU.

2. Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa viumbe vyote;

3. Mwingi wa Rehema Mwenye Kurehemu;

4. Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo.

5. Wewe tu tunakuabudu, na Wewe tu tunakuomba msaada.

6. Tuongoe njia iliyo nyooka,

7. Njia ya ulio waneemesha, siyo ya walio kasirikiwa, wala walio potea.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License