51 - 100
51. Enyi watu wangu! Sikuombeni ujira kwa ajili ya haya.
Haukuwa ujira wangu ila kwa Yule aliye niumba. Basi hamtumii akili?
52. Na enyi watu wangu! Muombeni msamaha Mola wenu Mlezi,
kisha mtubie kwake. Atakuleteeni mbingu zenye kunyesha mvua ya kumiminika, na
atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu. Wala msigeuke mkawa wakosefu.
53.
Wakasema: Ewe Hud! Hujatuletea dalili wazi. Wala sisi hatuiachi miungu
yetu kwa kufuata kauli yako. Na wala sisi hatukuamini wewe.
54. Sisi tunasema: Baadhi katika miungu yetu imekusibu kwa
baa. Akasema: Hakika mimi namshuhudisha Mwenyezi Mungu, na nyinyi shuhudieni,
ya kwamba mimi najitenga mbali na hao mnao wafanya washirika,
55.
Mkamwacha Yeye. Basi nyote nyinyi nipangieni vitimbi, na kisha msinipe muhula!
56. Hakika
mimi nimemtegemea Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wangu na Mola Mlezi wenu. Hapana
kiumbe yeyote ila Yeye anamwendesha atakavyo. Hakika Mola wangu Mlezi yuko juu
ya Njia Iliyo Nyooka.
57. Na
ikiwa watarudi nyuma, basi mimi nimekwisha kufikishieni niliyo tumwa kwenu. Na
Mola wangu Mlezi atawaleta watu wengine badala yenu, wala nyinyi hamumdhuru
kitu Yeye. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kuhifadhi kila kitu.
58. Ilipo
fika amri yetu, tulimwokoa Hud na walio amini pamoja naye, kwa rehema itokayo
kwetu. Na tukawaokoa na adhabu ngumu.
59. Na hao ndio kina A'adi. Walizikanusha Ishara za Mola
wao Mlezi, na wakawaasi Mitume wake, na wakafuata amri ya kila jabari mwenye
inda.
60. Na wakafuatishiwa laana katika dunia hii na Siku ya
Kiyama. Basi tambueni mtanabahi! Hakika kina A'adi walimkufuru Mola wao Mlezi. Na
tambueni mtanabahi kuwa hakika waliangamizwa kina A'adi, kaumu ya Hud.
61. Na kina Thamud tuliwapelekea ndugu yao Saleh. Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni
Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna
Mungu ila Yeye. Yeye ndiye aliye kuumbeni katika ardhi, na akakuwekeni humo.
Basi mwombeni msamaha, kisha mtubu kwake. Hakika Mola wangu Mlezi yupo karibu,
anaitikia maombi.
62.
Wakasema: Ewe Saleh! Hakika kabla ya haya ulikuwa unatarajiwa kheri kwetu. Je,
unatukataza tusiwaabudu waliyo kuwa wakiwaabudu baba zetu? Na hakika sisi tuna
shaka na wasiwasi kwa hayo unayo tuitia.
63.
Akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje ikiwa ninazo dalili zilizo wazi kutokana na
Mola wangu Mlezi, naye akawa kanipa rehema kutoka kwake - je, ni nani atakaye
ninusuru kwa Mwenyezi Mungu nikimuasi? Basi nyinyi hamtanizidishia ila
khasara tu.
64. Enyi watu
wangu! Huyu ngamia wa Mwenyezi Mungu ni Ishara kwenu. Basi mwacheni ale katika
ardhi ya Mwenyezi Mungu; wala msimguse kwa ubaya, isije ikakuangamizeni adhabu
iliyo karibu.
65.
Wakamchinja. Basi (Saleh) akasema: Stareheni katika mji wenu muda wa siku tatu.
Hiyo ni ahadi isiyo kuwa ya uwongo.
66. Basi
ilipo kuja amri yetu tulimwokoa Saleh na wale walio amini pamoja naye kwa
rehema yetu kutokana na hizaya ya siku ile. Hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye
nguvu Mwenye kushinda.
67. Na
ukelele uliwaangamiza wale walio dhulumu, wakapambazukiwa nao ni maiti
majumbani mwao.
68. Kama
kwamba hawakuwako huko. Hebu zingatieni! Hakika kina Thamud walimkufuru Mola
wao Mlezi. Hebu zingatieni! Thamud wamepotelea mbali!
69. Na wajumbe wetu walimjia Ibrahim kwa bishara njema,
wakasema: Salama! Naye akasema: Salama! Hakukaa ila mara akaleta ndama wa
kuchoma.
70. Basi alipoona mikono yao haimfikilii aliwatilia shaka,
na akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya Lut'.
71. Na mkewe alikuwa kasimama wima, akacheka. Basi
tukambashiria (kuzaliwa) Is-haq, na baada ya Is-haq Yaaqub.
72. Akasema: Je, hivyo mimi nizae, na hali yangu ni
kikongwe na huyu mume wangu ni kizee? Hakika haya ni mambo ya ajabu!
73. Wakasema: Je, unastaajabia amri ya Mwenyezi Mungu?
Rehema ya Mwenyezi Mungu na baraka zake ziko juu yenu, enyi watu wa nyumba hii!
Hakika Yeye ndiye Msifiwa wa kutukuzwa.
74. Basi khofu ilipo mwondoka Ibrahim, na ikawa ile bishara
imemfikia, alianza kujadiliana nasi juu ya kaumu ya Lut'.
75. Hakika Ibrahim alikuwa mpole, ana huruma, na mwepesi wa
kurejea kwa Mwenyezi Mungu.
76. (Akaambiwa): Ewe Ibrahim! Wachilia mbali haya! Kwa
hakika amri ya Mola wako Mlezi imekwisha kuja, na hakika hao itawafikia adhabu
isiyo rudi nyuma.
77. Na wajumbe wetu walipo kuja kwa Lut' aliwahuzunukia na
akawaonea dhiki. Akasema: Hii leo ni siku ngumu!
78. Wakamjia kaumu yake mbio mbio. Na kabla ya haya
walikuwa wakitenda maovu. Yeye akasema: Enyi watu wangu! Hawa binti zangu, ndio
wametakasika zaidi kwenu. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi mbele ya
wageni wangu. Hivyo, hamna hata mtu mmoja miongoni mwenu aliye ongoka?
79. Wakasema: Bila shaka umekwisha jua hatuna haki juu ya
binti zako, na unayajua tunayo yataka.
80. Akasema: Laiti ningeli kuwa na nguvu kwenu, au
nategemea kwenye nguzo yenye nguvu!
81.
(Wajumbe) wakasema: Ewe Lut'! Sisi ni wajumbe wa Mola wako Mlezi. Hawa
hawatakufikia. Na wewe ondoka pamoja na ahali zako usiku ungalipo. Wala yeyote
miongoni mwenu asitazame nyuma, isipo kuwa mkeo, kwani yeye utamfika msiba
utakao wafika hao. Hakika miadi yao ni asubuhi. Je, asubuhi si karibu?
82. Basi
ilipo fika amri yetu tuliigeuza nchi juu chini, na tukawateremshia mvua ya
changarawe za udongo mgumu ulio kamatana wa Motoni,
83. Zilizo
tiwa alama kwa Mola wako Mlezi. Na haya hayako mbali na wenye kudhulumu
wengineo.
84. Na kwa
watu wa Madyana tuliwatumia ndugu yao Shua'ib. Akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni
Mwenyezi Mungu. Nyinyi hamna Mungu ila Yeye, wala msipunguze vipimo na mizani.
Mimi nakuoneni mmo katika hali njema, nami nakukhofieni adhabu ya Siku kubwa
hiyo itakayo kuzungukeni.
85. Na enyi watu wangu! Timizeni vipimo na mizani kwa
uadilifu wala msiwakhini watu vitu vyao; wala msieneze uovu katika nchi
mkafanya uharibifu.
86. Alivyo kubakishieni Mwenyezi Mungu ndiyo bora kwa ajili
yenu, ikiwa nyinyi ni Waumini. Wala mimi siye mlinzi wenu.
87.
Wakasema: Ewe Shua'ibu! Ni sala zako ndizo zinazo kuamrisha tuyaache waliyo
kuwa wakiyaabudu baba zetu, au tuache kufanya tupendavyo katika mali zetu? Ama
hakika wewe ni mstahamilivu kweli na mwongofu!
88.
Akasema: Enyi watu wangu! Mwaonaje ikiwa ninayo dalili wazi inayo tokana na
Mola wangu Mlezi, na ikawa Yeye ameniruzuku riziki njema kutoka kwake? Wala
mimi sipendi kukukhalifuni nikafanya yale ninayo kukatazeni. Sitaki ila
kutengeneza kiasi ninavyo weza. Na sipati kuwezeshwa haya ila na Mwenyezi
Mungu. Kwake Yeye ninategemea, na kwake Yeye naelekea.
89. Na
enyi watu wangu! Kukhalifiana nami kusikupelekeeni hata mkasibiwa kama walivyo
sibiwa watu wa Nuhu, au watu wa Hud, au watu wa Saleh. Na watu wa Lut'
si mbali nanyi.
90. Na ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi, tena tubuni
kwake. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kurehemu na Mwenye upendo.
91.
Wakasema: Ewe Shua'ibu! Mengi katika hayo unayo yasema hatuyafahamu. Na
sisi tunakuona huna nguvu kwetu. Lau kuwa si jamaa zako tunge kupiga mawe, wala
wewe si mtukufu kwetu.
92. Akasema: Enyi watu wangu! Kwani jamaa zangu ni watukufu
zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu? Na Yeye mmemueka nyuma ya migongo yenu!
Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kuyazunguka yote mnayo yatenda.
93. Na enyi watu wangu! Fanyeni mwezayo, na mimi pia
ninafanya. Karibuni mtajua ni nani itakaye mfikia adhabu ya kumhizi, na nani
aliye mwongo. Na ngojeni, mimi pia ninangoja pamoja nanyi.
94. Na ilipo fika amri yetu, tulimwokoa Shua'ibu na wale
walio amini pamoja naye kwa rehema yetu. Na ukelele uliwanyakua walio dhulumu,
na wakapambaukiwa majumbani mwao wamekufa kifudifudi!
95. Kama kwamba hawakuwamo humo. Zingatia walivyo angamia
watu wa Madyana, kama walivyo angamia watu wa Thamud!
96. Na hakika tulimtuma Musa pamoja na Ishara zetu na
uthibitisho ulio wazi
97. Kwa Firauni na waheshimiwa wake. Lakini wao walifuata
amri ya Firauni, na amri ya Firauni haikuwa yenye uwongofu.
98. Siku ya Kiyama atawatangulia watu wake na atawaingiza
Motoni. Na muingio muovu ulioje huo!
99. Nao wamefuatishiwa laana hapa duniani na Siku ya
Kiyama. Ni mabaya yalioje watakayo pewa!
100. Hizi ni katika khabari za miji, tunakusimulia. Mingine
ipo bado na mingine imefyekwa.
|