101 - 111
101. Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika umenipa utawala, na
umenifunza tafsiri ya mambo. Ewe
Muumba wa mbingu na ardhi! Wewe ndiye Mlinzi wangu katika dunia na Akhera.
Nifishe hali ya kuwa ni Muislamu na nichanganyishe na watendao mema.
102. Hizi
ni katika khabari za ghaibu tulizo kufunulia. Na hukuwa pamoja nao walipo
azimia shauri yao, walipo fanya njama zao wakizua vitimbi.
103. Na wengi
wa watu si wenye kuamini hata ukijitahidi vipi..
104. Wala
wewe huwaombi ujira kwa haya. Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu
wote.
105. Na
ishara ngapi katika mbingu na ardhi wanazo zipitia, na hali ya kuwa
wanazipuuza.
106.Na
wengi katika wao hawamuamini Mwenyezi Mungu pasina kuwa ni washirikina.
107. Je!
Wanaaminisha kuwa haitowajia adhabu ya Mwenyezi Mungu ya kuwagubika, au
haitawafikia Saa ya Kiyama kwa ghafla, na hali hawatambui?
108. Sema:
Hii ndiyo Njia yangu - ninalingania kwa Mwenyezi Mungu kwa kujua - mimi na
wanao nifuata. Na ametakasika Mwenyezi Mungu! Wala mimi si katika washirikina.
109. Na
hatukuwatuma Mitume kabla yako isipo kuwa wanaume tulio wafunulia wahyi
miongoni mwa watu wa mijini. Je! Hawatembei katika ardhi wakaona jinsi ulivyo
kuwa mwisho wa walio kuwa kabla yao? Na hakika nyumba ya Akhera ni bora kwa
wamchao Mungu. Basi hamfahamu?
110. Hata
Mitume walipo kata tamaa na wakaona kuwa wamekadhibishwa, hapo ikawajia nusura
yetu, wakaokolewa tuwatakao. Na adhabu yetu haitowawacha kaumu ya wakosefu.
111. Kwa
hakika katika hadithi zao limo zingatio kwa wenye akili. Si maneno yaliyo
zuliwa, bali ni ya kusadikisha yaliyo kabla yake, na ufafanuzi wa kila kitu, na
ni uwongofu na rehema kwa kaumu yenye kuamini.
|