Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 15. SURATUL HIJR
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

15. SURATUL HIJR

(Imeteremka Makka)

Suratul Hijr ni Sura ya Makka. Nayo ina Aya 99. Imeanza kwa harufi za kutamkwa zenye kueleza kwamba Qur'ani imejengeka kwa harufi hizi hizi mnazo zitumia katika maneno yenu, na juu ya hivyo ni Muujiza kwenu, hamwezi kuleta kama hii. Kwani aliye iteremsha ni Mwenyezi Mungu, Aliye takasaika, na Akatukuka. Na hizo harufi pia ni kama kuwazindua wale wanao ipuuza Qur'ani, inawalingania, inawaita, waisikilize. Asaa wakanufaika, na wakahidika kumfuata Mwenyezi Mungu.
Sura hii tukufu inabainisha ili watu wazingatie yaliyo wapata kaumu zilizo tangulia, na khabari za Manabii walio kwisha pita, na yaliyo wapata kutokana na watu wao. Na pia Sura hii inaonyesha ishara za Mwenyezi Mungu katika ulimwengu, katika mbingu zilizo nyanyuliwa na zenye sayari ziilizo hifadhiwa, na ardhi iliyo tandikwa, na kukunjuliwa, na milima iliyo simama imara, na pepo zenye kubeba maji, na zenye kupandishia miti. Na Sura hii pia inaashiria mpambano wa mwanzo katika maumbile ya asli baina ya maluuni Iblisi na Adam na mkewe, na kuendelea mpambano huo baina ya kheri na shari mpaka imalizike dunia. Kisha tena malipo ya shari Siku ya Kiyama, na malipo ya kheri. Na baada ya hayo Mwenyezi Mungu anasimulia visa vya Manabii wawili, Ibrahim na Luut'i, na watu wa Al Hijr. Na Sura inaeleza cheo cha Qur'ani, na hali ya washirikina katika kuipokea, na impasavyo Nabii kwa mnasaba wa ukafiri wao, navyo ni kufikisha ujumbe wake, na kuutangaza, na kumuabudu Mwenyezi Mungu mpaka ifike amri ya yakini.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License