17. SURA AL ISRAAI (BANI ISRAIL)
(Imeteremka
Makka)
Sura
hii tukufu ina Aya 111, nayo ni Sura ya Makka ila Aya hizi: 26, 32, 33, 57 na
tangu Aya 73 mpaka Aya 80. Aya zote hizi, nazo ni 12, ni za Madina. Sura
hii imeanza kwa kumsabihi, kumtakasa, Mwenyezi Mungu Mtukufu. Kisha ikaitaja
Israi, nayo ni safari ya usiku aliyo chukuliwa Mtume s.a.w. kutoka Makka mpaka
Bait Al Muqaddas (Yerusalemu), na baadae akapelekwa mbinguni, na kurejeshwa
Makka usiku ule ule.
Baadae Sura inaeleza Ujumbe wa Nabii Musa a.s., na yaliyo kuwa ya Wana wa
Israili. Kisha ikaashiria cheo cha katika uwongofu, na zikatajwa Aya za uumbaji
usiku na mchana, na yatakayo watokea watu Siku ya Kiyama katika kulipwa kwa
vitendo walivyo vitenda duniani. Na Subhanahu amebainisha sababu za kuharibika
umma, na hali ya watu katika kuhangaika kwao, na matokeo ya vitendo vyao huko
Akhera. Tena zikaja Aya za kutukuzwa wazazi, baba na mama, na hali ya watu
kukhusu mali zao; na zikaja Amri Kumi za kuunda umma ulio bora. Kisha Subhanahu
akauvunja uzushi wa washirikina kukhusu Malaika, kisha akabainisha Qur'ani
inavyo eleza hoja zake.
Kisha Subhanahu akaashiria anavyo stahiki kuhimidiwa, na upinzani wa
washirikina, akawapa wasia Waumini. Na Mwenyezi Mungu Mtukufu akaeleza namna
anavyo watendea makafiri duniani na Akhera. Tena akaeleza asili ya uumbaji wa
binaadamu na Shet'ani, na akawatisha washirikina kwa Aya zake. Baada ya hayo
Subhanahu alibainisha utukufu wa binaadamu, na akataja adhabu za Siku ya
Kiyama. Akataja vipi washirikina wanavyo jaribu kumzuia Nabii asitimize Wito
wake, na vipi Mwenyezi Mungu anavyo mtia nguvu. Baada ya hayo Allahu Subhanahu
wa Taa'la akamuusia Nabii kwa wasia za uwongofu, na wito mnasaba. Kisha
akaashiria cheo cha , na akataja khabari za Roho, na akaashiria siri zake.
Kisha akataja umuujiza wa Qur'ani, kushindwa majini na watu kuleta mfano wake.
Na akabainisha Subhanahu uwezo wake kuleta Ishara nyengine. Tena akataja vipi
Qur'ani ilivyo kusanya Haki, na hali za Waumini wema katika Imani zao, na
inavyo takikana kuwa daima wawe wanamhimidi Mwenyezi Mungu na wakimtukuza
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|