Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 25. SURAT AL FURQAN
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

25. SURAT AL FURQAN

(Imeteremka Makka)

Idadi ya Aya za Sura hii ni 77. Zote ni za Makka isipo kuwa Aya 68, 69 na 70.
Sura imeanzia kwa kubainisha cheo cha Qur'ani, na ukubwa wa ufalme wa Mwenye kuiteremsha ambaye ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Na juu ya utukufu wa utawala wake, washirikina bado badala yake wanaabudu masanamu, na wanaikadhibisha Qur'ani, na wanaukataa Utume wa Mtume s.a.w. kwa hoja ya kuwa ati yeye ni binaadamu, anakula chakula, na anatembea masokoni, na kwa ubishi wanataka Malaika ndio wawaletee Ujumbe. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu amewafanya Mitume wake Malaika angeli wafanya ni watu ili wapate kufahamiana na watu. Ubabaishi unge baki. Na wakapinga kwa nini Qur'ani ikawa inateremka vipande vipande. Wakajibiwa hikima ya hayo. Na inda hii ikafuatilizwa kwa mifano yenye kueleza khabari za Mitume waliyo pita na kaumu zao. Lakini hizo kaumu zikafuata matamanio yao. Wakawa kama wanyama au wapotovu zaidi katika mwendo wao. Na zikaja Aya za uumbaji zenye kuonyesha ukamilifu wa kudra yake Mtukufu, yenye kufahamisha uangalizi na maarifa. Na Sura ikakhitimisha kwa kutaja sifa za Waumini zitazo warithisha vyumba vya Peponi vya juu, watapo pokewa kwa maamkio na kusalimiwa.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License