26. SURAT ASH-SHUA'RAA
(Imeteremka
Makka)
Sura hii imeanzia kwa
kuisifu Qur'ani yenyewe, ikaingia kuwaonya makafiri kwa uweza wa Mwenyezi Mungu
kuwateremshia adhabu juu yao, na kumliwaza Nabii s.a.w. kwa anayo yapata ya
kukanushwa na watu wake, kwa kutajiwa yalio wapata Mitume wa kabla yake ya
kukadhibishwa na kaumu zao. Ikasimulia mkutano wa Musa na Harun walipo kutana
na Firauni, na alivyo wakadhibisha yeye. Kisha Subhanahu akataja kisa cha
Ibrahim, baba wa Manabii, na khabari za Nuhu pamoja na kaumu yake, na mambo ya
A'adi, na Saleh pamoja na Thamud. Kisha ikaelezea Sura wito wa Lut'i na kisa
cha Shuaib na watu wa Vichakani (Al-Aykat).
Na mwenye kuzingatia visa vya hawa Manabii saba ataona asili ya wito wao ni
mmoja. Na njia ya makafiri katika kupinga ujumbe wao ni moja. Kama ilivyo anzia
Sura basi ilikhitimishia mazumgumzo kwa kuvunja wazo la kuwa Mtume ni mtunga
mashairi, na kuwa Qur'ani ni mashairi.
KWA JINA LA MWENYEZI
MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|