28. SURAT AL-QAS'AS'
(Imeteremka
Makka)
SURA YA AL-QAS'AS' ni ya 28
katika mpango wa Msahafu. Nayo
ni Sura ya Makka. Aya zake ni thamanini na nane.
Imetaja kwa kufafanua yaliyo kwisha tajwa kabla yake kwa jumla katika mambo ya
Musa a.s. tangu kuzaliwa kwake katika enzi ya Firauni. Na Firauni alikuwa
akiwauwa watoto wanaume wa Bani Israili kwa kukhofu asije tokea Nabii miongoni
mwao atakaye teketeza ufalme wake.
Kisha yakaelezwa yaliyo tokea kukhusu kulelewa kwake Musa katika nyumba ya
Firauni, mpaka alipo itoka Misri kukimbiza roho yake kwenda Madiani katika nchi
ya Shamu. Na tena akarejea na mkewe, binti wa Shuaibu a.s.
Kisha yakatajwa ya mazungumzo ya Mwenyezi Mungu na Musa, na kumteuwa yeye kwa
kumpa Utume, na mambo yaliyo tokea yaliyo mkhusu Firauni na wachawi wake pamoja
na Musa, mpaka Mwenyezi Mungu alipo mzamisha Firauni na jeshi lake. Na Musa na
Wana wa Israili walio kuwa pamoja naye wakaokoka. Kisha yaliyo watokea Wana wa
Israili pamoja na Musa na nduguye Harun. Na zimetajwa pia khabari za walio
kadhibisha kama Qaaruni na makafiri wengine walio watangulia. Na kwa maelezo
haya yaliyo kusanya khabari mbali mbali ndio Sura hii ikaitwa Surat al-Qas'as',
yaani Sura ya Visa, au Hadithi.
KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU
MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|