1 - 50
1. Ya-Sin
(Y.S.).
2. Kwa
Haki ya Qur'ani yenye hikima!
3. Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,
4. Juu ya Njia Iliyo Nyooka.
5. Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
6. Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao
wamekuwa wenye kughafilika.
7. Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi
katika wao, kwa hivyo hawaamini.
8. Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni.
Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.
9. Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na
tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.
10. Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.
11. Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na
akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na
ujira mwema.
12. Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo
yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli
lenye kubainisha.
13. Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio
tumwa.
14. Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi
tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa
kwenu.
15. Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi
mnasema uwongo tu.
16. Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi
tumetumwa kwenu.
17. Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.
18. Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa
hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka
kwetu.
19. Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu
walio pindukia mipaka.
20. Na akaja mtu
mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni
hawa walio tumwa.
21. Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa
wenyewe wameongoka.
22. NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake
mtarejeshwa?
23. Je!
Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia
madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.
24. Basi hakika
mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.
25. Hakika
mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!
26. Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu
wangeli jua
27. Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya
miongoni mwa walio hishimiwa.
28. Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka
mbinguni, wala si wenye kuteremsha.
29. Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!
30. Nawasikitikia
waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.
31. Je!
Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.
32. Na
hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.
33. Na Ishara
hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka,
wakawa wanazila!
34. Na
tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem
ndani yake,
35. Ili
wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?
36.
Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika
ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.
37. Na
usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.
38. Na jua
linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.
39. Na
mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.
40. Haliwi
jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia
zao.
41. Na ni
Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.
42. Na
tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.
43. Na
tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,
44. Isipo kuwa
kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.
45. Na
wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate
kurehemewa...
46. Na
haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye
kuipuuza.
47. Na
wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia
walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha
mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.
48. Na
wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?
49.
Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.
50. Basi
hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.
|