Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 36. SURAT YA-SIN
    • 1 - 50
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

1 - 50

1. Ya-Sin (Y.S.).

2. Kwa Haki ya Qur'ani yenye hikima!

3. Hakika wewe ni miongoni mwa walio tumwa,

4. Juu ya Njia Iliyo Nyooka.

5. Uteremsho wa Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.

6. Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa , basi wao wamekuwa wenye kughafilika.

7. Bila ya shaka kauli imekwisha thibiti juu ya wengi katika wao, kwa hivyo hawaamini.

8. Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu.

9. Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni.

10. Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini.

11. Hakika wewe unamwonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema.

12. Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha.

13. Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia walio tumwa.

14. Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazidishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu.

15. Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu.

16. Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu.

17. Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi.

18. Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu.

19. Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka.

20. Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa.

21. Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali ya kuwa wenyewe wameongoka.

22. NA KWA NINI nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?

23. Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa.

24. Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri.

25. Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!

26. Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua

27. Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio hishimiwa.

28. Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha.

29. Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!

30. Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli.

31. Je! Hawaoni umma ngapi tulizo ziangamiza kabla yao? Hakika hao hawarejei tena kwao.

32. Na hapana mmoja ila wote watakusanywa waletwe mbele yetu.

33. Na Ishara hiyo kwao - ardhi iliyo kufa, nasi tukaifufua, na tukatoa ndani yake nafaka, wakawa wanazila!

34. Na tukafanya ndani yake mabustani ya mitende na mizabibu, na tukatimbua chemchem ndani yake,

35. Ili wale matunda yake, na hayo hayakufanywa na mikono yao! Basi je, hawashukuru?

36. Subhana, Ametakasika, aliye umba dume na jike vyote katika vinavyo mea katika ardhi na katika nafsi zao, na katika wasivyo vijua.

37. Na usiku ni Ishara kwao. Tunauvua humo mchana, mara wao wanakuwa gizani.

38. Na jua linakwenda kwa kiwango chake. Hayo ni makadirio ya Mwenye nguvu, Mwenye kujua.

39. Na mwezi tumeupimia vituo, mpaka unakuwa kama karara kongwe.

40. Haliwi jua kuufikia mwezi, wala usiku kuupita mchana. Na vyote vinaogelea katika njia zao.

41. Na ni Ishara kwao kwamba Sisi tuliwapakia dhuriya zao katika jahazi ilio sheheni.

42. Na tukawaumbia kutoka mfano wake wanavyo vipanda.

43. Na tukitaka tunawazamisha, wala hapana wa kuwasaidia, wala hawaokolewi,

44. Isipo kuwa kwa rehema zitokazo kwetu na starehe kwa muda.

45. Na wanapo ambiwa: Jilindeni na yalioko mbele yenu na yalioko nyuma yenu, ili mpate kurehemewa...

46. Na haiwafikii Ishara yoyote katika Ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa ni wenye kuipuuza.

47. Na wanapo ambiwa: Toeni katika aliyo kupeni Mwenyezi Mungu, walio kufuru huwaambia walio amini: Je! Tuwalishe ambao Mwenyezi Mungu angependa angeli walisha mwenyewe? Nyinyi hammo ila katika upotofu ulio dhaahiri.

48. Na wanasema: Ahadi hii itatokea lini, ikiwa nyinyi ni wakweli?

49. Hawangojei ila ukelele mmoja tu utakao wachukua nao wamo kuzozana.

50. Basi hawataweza kuusia, wala kwa watu wao hawarejei.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License