Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 37. SURAT ASS'AFFAT
    • 1 - 50
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

1 - 50

1. Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.

2. Na kwa wenye kukataza mabaya.

3. Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.

4. Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.

5. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.

6. Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.

7. Na kulinda na kila shet'ani a'si.

8. Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.

9. Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.

10. Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.

11. Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.

12. Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.

13. Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.

14. Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.

15. Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.

16. Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?

17. Hata baba zetu wa zamani?

18. Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.

19. Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!

20. Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.

21. Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.

22. Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -

23. Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!

24. Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:

25. Mna nini? Mbona hamsaidiani?

26. Bali hii leo, watasalimu amri.

27. Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.

28. Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.

29. Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.

30. Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.

31. Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.

32. Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.

33. Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.

34. Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.

35. Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.

36. Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?

37. Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.

38. Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.

39. Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.

40. Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.

41. Hao ndio watakao pata riziki maalumu,

42. Matunda, nao watahishimiwa.

43. Katika Bustani za neema.

44. Wako juu ya viti wamekabiliana.

45. Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem

46. Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.

47. Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.

48. Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.

49. Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.

50. Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License