51 - 100
51. Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa
na rafiki
52. Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
53. Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio
tutalipwa na kuhisabiwa?
54. Atasema: Je! Nyie mnawaona?
55. Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
56. Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
57. Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka
ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
58. Je! Sisi hatutakufa,
59. Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi
hatutaadhibiwa.
60. Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
61. Kwa
mfano wa haya nawatende watendao.
62. Je!
Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
63. Hakika
Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
64. Hakika
huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
65.
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
66. Basi
hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
67. Kisha
juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
68. Kisha
hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
69. Hakika
waliwakuta baba zao wamepotea.
70. Na wao
wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
71. Na
bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
72. Na
Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
73. Basi
hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
74. Isipo
kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
75. Na
hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
76. Na
tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
77. Na
tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
78. Na
tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
79. Iwe
salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
80. Kwa hakika
hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
81. Hakika
yeye ni katika waja wetu walio amini.
82. Kisha
tukawazamisha wale wengine.
83. Na
hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
84. Alipo
mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
85.
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
86. Kwa
kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
87.
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
88. Kisha
akapiga jicho kutazama nyota.
89.
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
90. Nao
wakamwacha, wakampa kisogo.
91. Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona
hamli?
92. Mna nini hata hamsemi?
93. Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
94. Basi wakamjia upesi upesi.
95. Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
96. Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na
hivyo mnavyo vifanya!
97. Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni
humo!
98. Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao
ndio wa chini.
99. Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu
Mlezi; Yeye ataniongoa.
100. Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa
watenda mema.
|