Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 55. SURAT ARRAH'MAN
    • 1 - 50
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

1 - 50

1. Arrah'man, Mwingi wa Rehema

2. Amefundisha Qur'ani.

3. Amemuumba mwanaadamu,

4. Akamfundisha kubaini.

5. Jua na mwezi huenda kwa hisabu.

6. Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.

7. Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,

8. Ili msidhulumu katika mizani.

9. Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.

10. Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.

11. Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.

12. Na nafaka zenye makapi, na rehani.

13. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

14. Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..

15. Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.

16. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

17. Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.

18. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

19. Anaziendesha bahari mbili zikutane;

20. Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.

21. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

22. Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.

23. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

24. Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.

25. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

26. Kila kilioko juu yake kitatoweka.

27. Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

28. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

29. Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.

30. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

31. Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.

32. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

33. Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.

34. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

35. Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.

36. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

37. Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.

38. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

39. Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.

40. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

41. Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.

42. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

43. Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.

44. Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.

45. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

46. Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.

47. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

48. Bustani zenye matawi yaliyo tanda.

49. Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

50. Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License