Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 56. SURAT AL-WAAQIA'H
    • 51 - 100
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

51 - 100

51. Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

52. Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

53. Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

54. Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

55. Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

56. Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

57. Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

58. Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

59. Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

60. Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi 61. Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

62. Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

63. Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

64. Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

65. Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

66. Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

67. Bali sisi tumenyimwa.

68. Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

69. Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

70. Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

71. Je! Mnauona moto mnao uwasha?

72. Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

73. Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

74. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

75. Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

76. Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

77. Hakika hii bila ya shaka ni ,

78. Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

79. Hapana akigusaye ila walio takaswa.

80. Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

81. Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

82. Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

83. Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

84. Na nyinyi wakati huo mnatazama!

85. Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

86. Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

87. Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

88. Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

89. Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

90. Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

91. Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

92. Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

93. Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

94. Na kutiwa Motoni.

95. Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

96. Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License