93. SURAT WADH-DHUH'AA
(Imeteremka
Makka)
Sura hii imeanza kwa viapo
viwili vyenye kueleza nyakati mbili za uchangamfu na za kutulia, ya kwamba kwa
hakika Mwenyezi Mungu hakumwacha Mtume wake wala hakumchukia, na kwamba aliyo
mtengenezea katika Akhera makao ya juu ni bora zaidi kuliko alio mkirimu
duniani. Kisha Subhanahu akaapa kwamba Yeye atampa mpaka aridhike, na yaliyo
tangulia ni ushahidi wa yatakayo kuja. Kwani alikuwa yatima, akampatia makaazi;
alikuwa amepotea akampa bora ya uwongofu, na alikuwa fakiri akamtajirisha.
Kisha Aya zikataka aangaliwe vyema yatima, na asikemewe mwenye kuomba au
kuuliza, na zisimuliwe neema za Mwenyezi Mungu.
KWA JINA LA MWENYEZI
MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
1. Naapa kwa mchana!
2. Na kwa usiku unapo tanda!
3. Mola wako Mlezi hakukuacha, wala hakukasirika nawe.
4. Na bila ya shaka wakati ujao utakuwa bora kwako kuliko
ulio tangulia.
5. Na Mola wako Mlezi atakupa mpaka uridhike.
6. Kwani hakukukuta yatima akakupa makaazi?
7. Na akakukuta umepotea akakuongoa?
8. Akakukuta mhitaji akakutosheleza?
9. Basi yatima usimwonee!
10. Na anaye omba au kuuliza usimkaripie!
11. Na neema za Mola wako Mlezi zisimlie.
|