Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 99. SURAT AZ-ZILZALAH
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

99. SURAT AZ-ZILZALAH

(Imeteremka Madina)

Aya za Sura hii zote hazipindukii hali za Kiyama:-
Mtikisiko wa ardhi, na kutoka khazina na maiti walio zikwa chini, na kustaajabu kwa binaadamu na kuuliza kwake kwa yale yaliyo mkumba kwa ghafla, na kutoka watu makaburini mwao kwa mtafaruku wende kupokea malipo yao!

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!

2. Na itakapo toa ardhi mizigo yake!

3. Na mtu akasema: Ina nini?

4. Siku hiyo itahadithia khabari zake.

5. Kwa sababu Mola wake Mlezi ameifunulia!

6. Siku hiyo watu watatoka kwa mfarakano wakaonyweshwe vitendo vyao!

7. Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!

8. Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License