Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 103. SURAT AL-A'S'R
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

103. SURAT AL-A'S'R

(Imeteremka Makka)

Katika Sura hii anaapa Subhanahu kwa Zama, kwa zilivyo kusanya chungu ya ajabu, na mazingatio yenye kujuulisha uweza wa Mwenyezi Mungu na hikima yake, ya kwamba mtu haachi kuwa na upungufu katika vitendo vyake na hali zake ila Waumini wanao tenda mema, na wakausiana kushika Haki. Na hiyo ndiyo kheri yote. Na wakausiana kusubiri na kuvumilia juu ya walio amrishwa na walio katazwa.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Naapa kwa Zama!

2. Hakika binaadamu bila ya shaka yumo katika khasara,

3. Ila wale walio amini, na wakatenda mema, na wakausiana kwa haki, na wakausiana kusubiri.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License