Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 105. SURAT AL-FIIL
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

105. SURAT AL-FIIL

(Imeteremka Makka)

Mwenyezi Mungu anampa khabari Mtume wake s.a.w. kisa cha Watu wa Tembo (Ndovu) walio kusudia kuivunja Nyumba ya Mwenyezi Mungu ya Al-Kaa'ba, na anakionyesha kisa hichi kuwa ni dalili ya uweza wake Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kujilipizia kwake juu ya hao wanao vunja vitu vyake vitakatifu. Mwenyezi Mungu hakika aliwasalitishia majeshi yalio wang'oa mizizi yao, na wasibakie kitu ila kama nazi iliyo liwa na mwezi.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?

2. Kwani hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?

3. Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi,

4. Wakiwatupia mawe ya udongo wa Motoni,

5. Akawafanya kama majani yaliyo liwa!

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License