Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 109. SURAT AL-KAFIRUN
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

109. SURAT AL-KAFIRUN

(Imeteremka Makka)

Katika Sura hii Mwenyezi Mungu anamuamrisha Mtume wake s.a.w. awakatishe tamaa makafiri katika juhudi zao za kutaka kusikilizana na Mtume katika wito wake wa Haki, kwa kuwa yeye ni mwenye kubakia vile vile juu ya ibada ya Mwenyezi Mungu ambaye hapana mungu ila Yeye, na wao wabakie kuiabudu miungu yao ambayo haifidi chochote katika Haki, wao wawe na dini yao walio ifuata baba zao, na yeye na Dini yake aliyo mridhia Mwenyezi Mungu aifuate.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Sema: Enyi makafiri!

2. Siabudu mnacho kiabudu;

3. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

4. Wala sitaabudu mnacho abudu.

5. Wala nyinyi hamuabudu ninaye muabudu.

6. Nyinyi mna dini yenu, nami nina Dini yangu.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License