Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 111. SURAT AL-MASAD
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

111. SURAT AL-MASAD

(Imeteremka Makka)

Sura imeanza kwa kutoa khabari kuhiliki kwa Abu Lahab, adui wa Mwenyezi Mungu na Mtume wake, na kuwa hapana kitu cha kumfaa, mali wala cheo au vyenginevyo, na inamuahidi kuwa Akhera ataingia Motoni na ataungua humo, pamoja na mkewe ataye kuwa naye. Na yeye amekhusishwa kwa adhabu ya kufungwa kamba katika shingo yake ya kumvutia mpaka kwenye Moto katika kuzidi kumuadhibu kwa sababu ya maudhi yake aliyo kuwa akimfanyia Mtume na maovu aliyo kuwa akiyafanya kupinga Wito.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Imeangamia mikono ya Abu Lahab, na yeye pia ameangamia.

2. Hayatamfaa mali yake, wala alivyo vichuma.

3. Atauingia Moto wenye mwako.

4. Na mkewe, mchukuzi wa kuni,

5. Shingoni mwake iko kamba iliyo sokotwa.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License