Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 113. SURAT AL-FALAQ
Previous - Next

Click here to hide the links to concordance

113. SURAT AL-FALAQ

(Imeteremka Makka)

Sura hii inamtaka Nabii s.a.w. amwendee Mola wake Mlezi atake ulinzi kwake kujilinda na shari ya kila mwenye shari, ya viumbe vyake, na shari za usiku linapo ingia giza, yanayo yasibu nafsi katika hali ya upweke, na madhara ambayo mtu hawezi kujikinga nayo, na shari za mafisadi wanao pita kuharibu makhusiano na mawasiliano yalio baina ya watu, na shari za hasidi anaye tamani kuondoa neema alizo wapa Mwenyezi Mungu waja wake.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko,

2. Na shari ya alivyo viumba,

3. Na shari ya giza la usiku liingiapo,

4. Na shari ya wanao pulizia mafundoni,

5. Na shari ya hasidi anapo husudu.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License