Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Qu'rani IntraText CT - Text |
|
|
9. SURATUT TAWBA (Imeteremka Madina) Suratut
Tawba iliteremka Madina katika mwaka wa tisa wa Hijra, yaani miaka tisa baada
ya Mtume s.a.w. kuhamia Madina. Akaichukua Sura hii Ali bin Abi Talib r.a.
kuwapelekea Waislamu katika Hija na akawasomea. Na amir, yaani mwongozi, wa
Hija hiyo alikuwa Abu Bakr Assidiq r.a. Na Aya zake ni 129. Imeanzia kwa
kujitenga Mwenyezi Mungu Mtukufu na washirikina. Na kwa hivyo ikaitwa pia Sura
ya Baraa-ah, yaani kujitenga, kutokuwa na dhima, kutokuwa na jukumu. Na baada
ya hayo ikataja utakatifu wa miezi mitakatifu, na ahadi za washirikina, na
ipasavyo kutimiza ahadi nao ikiwa wao hawajaivunja. Na mwenye kuvunja ahadi
yapasa kupigana naye. Na baada ya hayo ikabainisha kuwa kiini cha kutaka
kumkaribia Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kumuamini Yeye. Na Imani haikamiliki ila
akiwa Mwenyezi Mungu na Mtume wake wanapendwa na Waumini kuliko kila kitu. Naye
Subhanahu ametaja kuwa kujiona una nguvu ndio kunapelekea kuwa mbali ushindi,
na akaashiria mfano wa vita vya Hunayni. Katika Sura hii wamepigiwa marfuku
washirikina wasiingie katika Msikiti Mtakatifu wa Makka, kwa kuwa wao ni
najisi!
|
Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License |