Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 11. SURAT HUD
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

11. SURAT HUD

(Imeteremka Makka)

Surat Hud ni Sura ya Makka. Ina Aya 123. Imeanza kwa kuisifu , na kumuabudu Mwenyezi Mungu peke yake, na kuonya, na kubashiria. Kisha ikabainisha uwezo wa Mwenyezi Mungu na kuwa Yeye ndiye Mola Mlezi. Na ikaeleza hali za watu katika kuzipokea kwao neema zake Mola Mlezi, na adhabu zake. Kisha ikataja cheo cha Qur'ani, na kufuru za makafiri bila ya udhuru wowote kwa ukafiri wao, na malipo ya Waumini.
Naye Subhanahu baada ya hayo amesimulia hadithi za Manabii, na majadiliano ya kaumu zao nao, na kuwateremkia makafiri adhabu ya duniani na kuokoka kwa Waumini. Subhanahu wa Taa'la akataja hadithi ya Nuhu kwa kupambanua zaidi kuliko ilivyo kuwa katika Surat Yunus. Humu imeelezwa fikra za kafiri na inadi yake, na imebainishwa ilivyo mteremkia chuki. Na baada ya hadithi ya Nuhu Mwenyezi Mungu Subhanahu ametaja kisa cha A'ad pamoja na Nabii wa Mwenyezi Mungu Hud, kwa kueleza wazi mawazo ya ukafiri, na yaliyo wateremkia makafiri juu ya kuwa walikuwa na nguvu na wakali.
Kisha kikatajwa mfano wa hayo kisa cha Nabii wa Mwenyezi Mungu, Saleh pamoja na kabila la Thamud, na tena kisa cha Nabiyyu Llah na rafiki yake, Ibrahim. Kisha hadithi wa Nabiyyu Llah, Lut'. Kisha kisa cha Nabiyyu Llah, Shua'ib.
Kisha Subhanahu wa Taala ametaja nini mafunzo ya hadithi hizi za kweli, na akamalizia Subhanahu kwa kuwataka Waumini watende mema, na wangojee malipo. Tena ukatajwa ujuzi ulio kamilika wa Mwenyezi Mungu Aliye takasika na kutukuka, na waajibu wa kumtegemea Yeye.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License