Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 12. SURAT YUSUF
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

12. SURAT YUSUF

(Imeteremka Makka)

Sura hii ni ya Makka, na Aya zake ni mia na kumi na moja. Ndani yake Mwenyezi Mungu amesimulia hadithi ya Yusuf katika Aya tisiini na nane, na ameitangulizia kwa Aya tatu alizo taja ndani yake huu ufunuo alio mteremshia Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu na amani zishuke juu yake. Na ameuita ufunuo huu katika Aya ya kwanza: Kitabu kinacho bainisha. Na katika Aya ya pili akauiita: Qur'ani kwa Kiarabu, kuwa ni kuashiria kwamba ni haki yake uhifadhiwe kwa maandishi na katika vifua vya watu vile vile. Kisha katika Aya ya tatu akataja kuwa ufunuo huu umekusanya simulizi nzuri kabisa, na ukataja kuwa Nabii Muhammad hakuwa akiyajua hayo kabla hakuteremshiwa huo Wahyi (ufunuo). Na hiyo ni dalili kuwa haya yanatoka kwa Mwenyezi Mungu. Na kisa hichi na Sura hii imemalizikia kwa kutilia mkazo yaliyo anzia. Na akamuelekeza Nabii mnamo Aya kumi azingatie kuwa masimulizi haya ni katika khabari za ghaibu, ambazo yeye Nabii, Salla Llahu alayhi wasallama, hakuwa akizijua, na kuzijua ukweli wake zilivyo, kabla ya kuteremshiwa Wahyi. Wala yeye hakuwa pamoja na hao ndugu zake Yusuf walipo kuwa wakipanga mipango yao, na wakiunda njama zao za shari kumuundia ndugu yao kwa baba. Kisha Qur'ani inamwambia Mtume kuwa inda na husda huwapelekea watu wengi kuingia ukafirini. Na kwamba pupa yake Mtume s.a.w. kuwa waamini wengi wao haitomfalia kitu, lakini Qur'ani inampoza kwa hayo kwa kuwa yeye hataki ujira, ila ni kuwa yeye anawaletea Qur'ani iwe ni uwongofu na ukumbusho kwa watu wote. Na mwisho wa Sura inaashiria Mitume ambao hadithi zao zimesimuliwa, na ukasimuliwa msimamo wa kaumu zao, na vipi mwishoe walivyo washinda makafiri wakosefu. Na katika hadithi hizi za Manabii pana mazingatio kwa wenye akili. Hakika hii Qur'ani inayo simulia masimulio haya na mengineyo si kitu cha kutungwa tu na kuzuliwa kuwa kinatoka kwa Mwenyezi Mungu kwa uwongo. Hakika hii ni haki na kweli tupu, na hichi ni Kitabu kinacho sadikisha Vitabu sahihi vilivyo toka mbinguni, na ni uwongofu, na rehema kwa watu wanao zingatia na wakaamini.
Linalo onekana wazi katika sifa za Sura hii ni kuwa kimesimuliwa kisa cha Yusuf kwa ukamilifu wake. Na pia imeonekana kuwa katika ule ule ukoo mmoja upo uhasidi ulio enea na pia katika baadhi yao yapo mapenzi. Husda ya wana wa Yaaqub iliwapelekea kumtumbukiza ndugu yao kisimani. Lakini Mwenyezi Mungu alimlinda na vitimbi vyao, kama alivyo mkinga na matamanio ya mke wa Mheshimiwa pale Yusuf alipo fikilia utuuzima nyumbani kwa Mheshimiwa. Mwenyezi Mungu akamweka vizuri katika nchi ya Misri, na akamjaalia kuwa nchi hiyo iwe makimbilio (mategemeo) ya wale walio mpangia njama za kumdhuru. Basi ni hivyo shani yake Subhanahu wa Taa'la kwa Manabii wake na vipenzi vyake. Huwanusuru dhidi ya maadui zao, na huwathibitisha na kuwaweka vyema katika ardhi maadamu wanaishika Haki na wanaiamini, na wanaishikilia kamba ya Mwenyezi Mungu.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License