Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Qu'rani IntraText CT - Text |
|
|
12. SURAT YUSUF (Imeteremka Makka) Sura
hii ni ya Makka, na Aya zake ni mia na kumi na moja. Ndani yake Mwenyezi Mungu
amesimulia hadithi ya Yusuf katika Aya tisiini na nane, na ameitangulizia kwa
Aya tatu alizo taja ndani yake huu ufunuo alio mteremshia Muhammad, rehema za
Mwenyezi Mungu na amani zishuke juu yake. Na ameuita ufunuo huu katika Aya ya
kwanza: Kitabu kinacho bainisha. Na katika Aya ya pili akauiita: Qur'ani kwa
Kiarabu, kuwa ni kuashiria kwamba ni haki yake uhifadhiwe kwa maandishi na
katika vifua vya watu vile vile. Kisha katika Aya ya tatu akataja kuwa ufunuo
huu umekusanya simulizi nzuri kabisa, na ukataja kuwa Nabii Muhammad hakuwa
akiyajua hayo kabla hakuteremshiwa huo Wahyi (ufunuo). Na hiyo ni dalili kuwa
haya yanatoka kwa Mwenyezi Mungu. Na kisa hichi na Sura hii imemalizikia
kwa kutilia mkazo yaliyo anzia. Na akamuelekeza Nabii mnamo Aya kumi azingatie
kuwa masimulizi haya ni katika khabari za ghaibu, ambazo yeye Nabii, Salla
Llahu alayhi wasallama, hakuwa akizijua, na kuzijua ukweli wake zilivyo, kabla
ya kuteremshiwa Wahyi. Wala yeye hakuwa pamoja na hao ndugu zake Yusuf walipo
kuwa wakipanga mipango yao, na wakiunda njama zao za shari kumuundia ndugu yao
kwa baba. Kisha Qur'ani inamwambia Mtume kuwa inda na husda huwapelekea watu
wengi kuingia ukafirini. Na kwamba pupa yake Mtume s.a.w. kuwa waamini wengi
wao haitomfalia kitu, lakini Qur'ani inampoza kwa hayo kwa kuwa yeye hataki
ujira, ila ni kuwa yeye anawaletea Qur'ani iwe ni uwongofu na ukumbusho kwa
watu wote. Na mwisho wa Sura inaashiria Mitume ambao hadithi zao zimesimuliwa,
na ukasimuliwa msimamo wa kaumu zao, na vipi mwishoe walivyo washinda makafiri
wakosefu. Na katika hadithi hizi za Manabii pana mazingatio kwa wenye akili.
Hakika hii Qur'ani inayo simulia masimulio haya na mengineyo si kitu cha
kutungwa tu na kuzuliwa kuwa kinatoka kwa Mwenyezi Mungu kwa uwongo. Hakika hii
ni haki na kweli tupu, na hichi ni Kitabu kinacho sadikisha Vitabu sahihi vilivyo
toka mbinguni, na ni uwongofu, na rehema kwa watu wanao zingatia na wakaamini. KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|
Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License |