Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Qu'rani IntraText CT - Text |
|
|
18. SURA AL KAHF (Imeteremka Makka) Sura
hii ni ya Makka, isipo kuwa Aya 38, na Aya zinazo anzia 83 mpaka 101. Basi
zimo Aya ishirini za Madina. Nayo imeanzia kwa kumhimidi Mwenyezi Mungu Mtukufu
kwa kuiteremsha , na kubainisha kuwa Qur'ani ni onyo na bishara. Ndani yake
lipo onyo kwa wanao dai kuwa ati Mwenyezi Mungu ana mwana. Na humu imetajwa
hamu kubwa aliyo nayo Nabii ya kutaka waamini wale anao waita kwenye mlingano
wa Mwenyezi Mungu. Kisha kikatajwa kisa cha Ahlil Kahf, Watu wa Pangoni, walio
lala usingizi kisha wakaamka baada ya kukaa katika pango lao muda wa miaka mia
tatu na tena wakazidishiwa tisa. Na watu hao walikuwa Wakristo walio kuwa
wakikimbia udhalimu wa mtawala wa Kirumi. Wakalala katika pango muda huo, kisha
wakaamka ili kuwa ni ishara ya uweza wa Mwenyezi Mungu Mtukufu kufufua baada ya
kufa. KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|
Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License |