Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Qu'rani IntraText CT - Text |
|
|
20. SURAT T'AHA (Imeteremka Makka) SURA
HII ni ya Makka, isipo kuwa Aya mbili, nazo ni Aya 130 na 131. Hisabu ya Aya zake ni 135. Sura hii
imeanza kwa harufi mbili za kuzindua juu ya muujiza wa Qur'ani, na kuwazindua wasikilizaji
waisikilize. Baada ya harufi hizo mbili cheo cha Qur'ani kimetajwa, na utukufu
wa hii Qur'ani ni utukufu wa Mwenye kuileta, naye ni Mwenyezi Mungu, Subhanahu
wa Taa'la, Mmiliki mbingu na ardhi, Mwenye kujua siri, na kilicho fichikana
kuliko siri. Kisha kimesimuliwa kisa cha Musa a.s. pamoja na Firauni, na vipi
alipo anza kupewa utume Nabii Musa a.s. Na yametajwa maombi yake kutaka nduguye
Harun a.s. awe msaidizi wake wa kumpa nguvu, tena vipi walivyo kutana na
Firauni baada ya kitisho cha mkutano wake kwa ajili ya ujeuri wake. Na katika
mintarafu ya haya Mwenyezi Mungu Mtukufu amebainisha kuzuka kwa Musa a.s. KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|
Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License |