Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 26. SURAT ASH-SHUA'RAA
    • 101 - 150
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

101 - 150

101. Wala rafiki wa dhati.

102. Laiti tungeli pata kurejea tena tungeli kuwa katika Waumini.

103. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

104. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

105. Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume.

106. Alipo waambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamchimngu?

107. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

108. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

109. Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

110. Basi Mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

111. Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanao kufuata ni watu wa chini?

112. Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?

113. Hisabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!

114. Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini.

115. Mimi si cho chote ila ni Mwonyaji wa dhaahiri shaahiri.

116. Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe.

117. Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha.

118. Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini.

119. Kwa hivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni.

120. Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia.

121. Hakika katika haya ipo Ishara, lakini si wengi wao walio kuwa Waumini.

122. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

123. Kina A'd waliwakanusha Mitume.

124. Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamchimngu?

125. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

126. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.

127. Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

128. Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?

129. Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!

130. Na mnapo tumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari.

131. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

132. Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua.

133. Amekupeni wanyama wa kufuga na wana.

134. Na mabustani na chemchem.

135. Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku Kubwa.

136. Wakasema: Ni mamoja kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha.

137. Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani.

138. Wala sisi hatutaadhibiwa.

139. Wakamkanusha; nasi tukawaangamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini.

140. Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu.

141. Kina Thamud waliwakanusha Mitume.

142. Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchimngu?

143. Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu.

144. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini.

145. Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

146. Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?

147. Katika mabustani, na chemchem?

148. Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva.

149. Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi.

150. Basi mcheni Mwenyezi Mungu, na nit'iini mimi.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License