Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Qu'rani IntraText CT - Text |
|
|
30. SURAT AR-RUM (Imeteremka Makka) SURA hii imeanza kutaja
kushindwa kwa dola ya Rumi, na ahadi ya Mwenyezi Mungu kwa Waumini kwamba
atawapa ushindi kuwashinda Waajemi, na ikawataka watu wafikiri juu ya uumbaji
wa Mwenyezi Mungu, na watembee katika ardhi wapate kuujua mwisho wa makafiri
walio iamirisha ardhi zaidi kuliko walivyo iamirisha wao Makureshi. Na Sura hii
imeeleza hali ya watu Siku ya Kiyama, na ikasifu kutakasa kwa Waumini kumtakasa
Mwenyezi Mungu, na wanavyo muabudu Yeye asubuhi mapema na jioni, na adhuhuri na
alasiri. Na ikanabihisha dalili za Upweke wake Mwenyezi Mungu kwa kupishana zamu
usiku na mchana, na kukhitalifiana lugha, na mambo yanayo onekana ya ulimwengu
katika mbingu na ardhi. Na ikapiga mifano ambayo inayo onyesha upotovu wa
shirki, na ikawakumbusha watu vipi Mwenyezi Mungu alivyo waumba wao na
akawaneemesha, na kuvitia nguvu viungo vya ukoo, na kushikamana kwa ujamaa, na
ikashughulikia mambo ya sharia, ikaharimisha riba, na ikalazimisha Zaka, na
ikahimiza kuwafanyia wema jamaa. KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
|
Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library |
Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License |