101 - 150
101. Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
102. Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja
naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa
ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo
amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
103. Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu
ya kipaji.
104. Tulimwita: Ewe Ibrahim!
105. Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo
walipa wanao tenda mema.
106. Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
107. Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
108. Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja
baadaye.
109. Iwe
salama kwa Ibrahim!
110. Hivi
ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
111.
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
112. Na
tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
113. Na
tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na
wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
114. Na
kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
115. Na
tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
116. Na
tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
117. Na
tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
118. Na
tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
119. Na
tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
120. Iwe salama kwa Musa na Haruni!
121. Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
122. Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
123. Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa
Mitume.
124. Alipo
waambia watu wake: Hamwogopi?
125.
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
126.
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
127.
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
128. Isipo
kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
129. Na tumemwachia
(sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
130. Iwe
salama kwa Ilyas.
131.
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
132.
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
133. Na
hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
134.
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
135. Isipo
kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
136. Kisha
tukawaangamiza wale wengineo.
137. Na
hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
138. Na usiku. Basi
je! Hamyatii akilini?
139. Na hakika
Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
140. Alipo
kimbia katika jahazi lilio sheheni.
141. Akaingia
katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
142. Samaki
akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
143. Na ingeli
kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
144. Bila ya shaka
angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
145. Lakini
tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
146. Na
tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
147. Na
tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
148. Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
149. Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto
wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
150. Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao
wakashuhudia?
|