51 - 88
51. Humo wataegemea matakia, wawe wanaagiza humo matunda
mengi na vinywaji.
52. Na pamoja nao wake zao wenye kutuliza macho, hirimu
zao.
53. Haya ndiyo mliyo ahidiwa kwa Siku ya Hisabu.
54. Hakika hii ndiyo riziki yetu isiyo malizika.
55. Ndio hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata
marudio maovu kabisa;
56. Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni
kitanda kiovu mno cha kulalia.
57. Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!
58. Na adhabu nyenginezo za namna hii.
59. Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana
makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni.
60. Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi
ndio mlio tusabibisha haya, napo ni pahala paovu kabisa!
61. Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusabibisha haya
mzidishie adhabu mara mbili Motoni.
62. Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao
tukiwahisabu ndio katika waovu?
63. Tulikosea tulipo wafanyia maskhara, au macho yetu tu
hayawaoni ?
64. Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa
Motoni.
65. Sema: Hakika mimi ni mwonyaji tu; na hapana mungu ila
Mwenyezi Mungu Mmoja, Mtenda nguvu,
66. Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na viliomo baina yake,
Mwenye nguvu, Mwenye kusamehe.
67. Sema: Hii ni khabari kubwa kabisa.
68. Ambayo
nyinyi mnaipuuza.
69. Sikuwa
na ilimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipo kuwa wakishindana.
70.
Haikufunuliwa kwangu isipo kuwa ya kwamba hakika mimi ni mwonyaji dhaahiri.
71. Mola
wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitaumba mtu kutokana na udongo.
72. Na
nitakapo mkamilisha na kumpulizia roho inayo tokana nami, basi muangukieni kwa
kumt'ii.
73. Basi
Malaika wakat'ii wote pamoja.
74. Isipo
kuwa Iblisi; alijivuna na akawa katika makafiri.
75.
Mwenyezi Mungu akamwambia: Ewe Iblisi! Kipi kilicho kuzuia kumt'ii yule niliye
muumba kwa mikono yangu? Je!
Umejiona mkubwa, au umekuwa katika wakuu kweli?
76. Akasema: Mimi ni bora kuliko yeye. Umeniumba kwa moto,
na yeye umemuumba kwa udongo.
77. Akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe umelaanika.
78. Na hakika laana yangu itakuwa juu yako mpaka Siku ya
Malipo.
79. Akasema: Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku
watayo fufuliwa viumbe.
80. Mwenyezi Mungu akasema: Basi umekwisha kuwa miongoni
mwa walio pewa muhula,
81. Mpaka siku ya wakati maalumu.
82. Akasema (Iblisi): Naapa kwa utukufu wako, bila ya shaka
nitawapoteza wote,
83. Isipo kuwa wale waja wako miongoni mwao walio
khitariwa.
84. Akasema: Haki! Na haki ninaisema.
85. Bila ya shaka nitaijaza Jahannamu kwa wewe na kwa hao
wote wenye kukufuata miongoni mwao.
86. Sema (Ewe Mtume) : Sikuombeni ujira juu ya haya, wala
mimi si katika wadanganyifu.
87. Hayakuwa haya ila ni mawaidha kwa walimwengu wote.
88. Na bila ya shaka mtajua khabari zake baada ya muda.
|