Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 56. SURAT AL-WAAQIA'H
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

56. SURAT AL-WAAQIA'H

(Imeteremka Makka)

Sura hii imeanzia kwa kusimulia Tukio la Kiyama, na matokeo yatayo ambatana na Tukio hilo. Kisha ikasimulia kuwa viumbe Siku hiyo watakuwa namna tatu. Ikafuatia hayo kwa kufafanua kwa kutosha walio andaliwa kila fungu katika hao, ikiwa ni neema zinazo wafikiana na cheo chao, au ni adhabu inayo nasibiana na ukafiri wao na uasi wao.
Kisha Aya zikaweka wazi baada ya hayo yanayo onekana katika neema za Mwenyezi Mungu Mtukufu, na athari za uweza wake katika viumbe, na makulima, na maji, na moto; na yanayo hitajika kutokana na athari hizi kumsabihi Mwenyezi Mungu Mtukufu na kumtakasa.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Litakapo tukia hilo Tukio

2. Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

3. Literemshalo linyanyualo,

4. Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

5. Na milima itapo sagwasagwa,

6. Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

7. Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

8. Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

9. Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

10. Na wa mbele watakuwa mbele.

11. Hao ndio watakao karibishwa

12. Katika Bustani zenye neema.

13. Fungu kubwa katika wa mwanzo,

14. Na wachache katika wa mwisho.

15. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

16. Wakiviegemea wakielekeana.

17. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

18. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

19. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

20. Na matunda wayapendayo,

21. Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

22. Na Mahurulaini,

23. Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

24. Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

25. Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

26. Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

27. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

28. Katika mikunazi isiyo na miba, 29. Na migomba iliyo pangiliwa,

30. Na kivuli kilicho tanda, 31. Na maji yanayo miminika,

32. Na matunda mengi,

33. Hayatindikii wala hayakatazwi,

34. Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

35. Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

36. Na tutawafanya vijana,

37. Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

38. Kwa ajili ya watu wa kuliani.

39. Fungu kubwa katika wa mwanzo,

40. Na fungu kubwa katika wa mwisho. 3

41. Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

42. Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

43. Na kivuli cha moshi mweusi,

44. Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

45. Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

46. Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa, 47. Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

48. Au baba zetu wa zamani?

49. Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

50. Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License