Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 97. SURAT AL-QADR
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

97. SURAT AL-QADR

(Imeteremka Makka)

Katika Sura hii inasifiwa shani ya Qur'ani na shani ya Usiku ilipo teremshwa Qur'ani, na inaelezwa kwamba usiku huo mmoja ni bora kuliko miezi elfu, na kwamba hakika Malaika na Jibrili huteremka usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa ajili ya kila amri, kwa kusalimika na kila maudhi na uovu mpaka kuchomoza alfajiri yake.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.

2. Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?

3. Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

4. Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.

5. Amani usiku huo mpaka mapambazuko ya alfajiri.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License