Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 106. SURAT QURAISH
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

106. SURAT QURAISH

(Imeteremka Makka)

Mwenyezi Mungu katika Sura hii anataja neema alizo wafanyia Maqureshi kwa Nyumba yake takatifu ambayo ameilinda na maadui wake, naye akawapa maskani karibu yake wakapata utukufu na amani, na wakawa wanasafiri siku za baridi kwenda Yaman, na siku za joto wakenda Shamu, kwa ajili ya biashara bila ya mtu yeyote kuwaletea maovu, na hali watu jirani zao siku zote wakinyakuliwa. Na neema hizo zinawajibikia kumuabudu huyo aliye kuwa anawalisha wasipate njaa, na akawalinda na khofu.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Kwa walivyo zoea Maqureshi,

2. Kuzoea kwao safari za siku za baridi na siku za joto.

3. Basi nawamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii,

4. Ambaye anawalisha wasipate njaa, na anawalinda na khofu.




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License