Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 107. SURAT AL-MAAU'N
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

107. SURAT AL-MAAU'N

(Imeteremka Makka)

Sura hii inahadithia khabari za mwenye kukadhibisha malipo ya Akhera. Ikataja katika sifa zake kuwa yeye anamdhalilisha yatima, na anamkemea kwa ukali, si kwa kumtengeza. Na kwamba yeye hamhimizi mtu yeyote, la kwa kauli wala kwa kitendo, kuwalisha masikini; kwa sababu huyo ni mchoyo kwa mali yake, bakhili kwa alicho nacho mkononi. Kisha Sura imewataja watu wa kikundi kingine wanao shabihiana na hawa wanao kadhibisha malipo. Hawa ni wale wanao ghafilika na Sala zao, ambao hawasali kama itakikanavyo, na ambao husimama kwa hayo kwa dhaahiri tu si kwa hakika. Ni wenye kuonyesha tu a'mali zao, wenye kuzuia msaada wao wasiwape wanao hitajia. Na Sura inawaahidi hao kuwa watapata misiba na maangamio, ili waache uasi wao.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Je! Umemwona anaye kadhibisha Malipo?

2. Huyo ndiye anaye msukuma yatima,

3. Wala hahimizi kumlisha masikini.

4. Basi, ole wao wanao sali,

5. Ambao wanapuuza Sala zao;

6. Ambao wanajionyesha,

7. Nao huku wanazuia msaada.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License