Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 110. SURAT ANNAS'R
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

110. SURAT ANNAS'R

(Imeteremka Madina)

Sura hii imemtaka Mtume wa Mwenyezi Mungu s.a.w. ukija msaada wa Mwenyezi Mungu na ushindi, na akaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi kwa kutua mambo yake na kutukuka neno lake na kumkamilishia Mwenyezi Mungu, basi amtakase Mola wake Mlezi kwa kumsifu, na amtakase na kila lisio mwelekea, na amwombe msamaha kwa nafsi yake na kwa Waumini, kwa sababu hakika Yeye ni Mwingi wa kukubali toba za waja wake, na anasamehe makosa.

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

1. Itakapo kuja nusura ya Mwenyezi Mungu na ushindi,

2. Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Mwenyezi Mungu kwa makundi,

3. Zitakase sifa za Mola wako Mlezi, na umwombe msamaha; hakika Yeye ndiye anaye pokea toba.

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License