Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Qu'rani

IntraText CT - Text

  • 6. SURAT AL - AN-A'AM
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

6. SURAT AL - AN-A'AM

(Imeteremka Makka)

SURA hii ni ya Makka isipo kuwa Aya hizi: 20, 23, 91, 93, 114, 141, 151, 152, na 153. Na Aya zake ni 165. Iliteremka baada ya Sura Al-Hijr. Na Sura hii tukufu imekusanya maana zilizo wekwa mbali mbali kama ifuatavyo:

Imewazindua watu wauzingatie ulimwengu na dalili ziliomo ndani yake zenye kuonyesha Ubora wa aliye uumba, na Utukufu wake na Umoja wake wa pekee, na kuwa Yeye hashirikiani na yeyote, la katika kuumba, wala katika kuabudiwa, wala katika dhati yake.

Na imekusanya visa vya baadhi ya Manabii, na ikaanza kwa kisa cha Ibrahim a.s. kwa kubainisha kuwa alichukua maana ya ibada na Tawhidi kwa kuuchungua ulimwengu, na kufuata yaliyomo ndani yake. Naye alianza kwa kupeleleza nyota, kisha mwezi, kisha jua, na akamalizia kwa kufuata ibada ya Mwenyezi Mungu peke yake.

Na ikapelekea macho yaangalie ajabu za uumbaji na vipi mambo yanavyo kuwa. Ikabainisha vipi kilicho hai kinyevu kinatokana na kisicho kuwa na uhai kikavu; na vipi mbegu inavyo pasuka na ukachipua mmea.

Na Sura hii imezitaja sifa za wapinzani, na vipi wanavyo shikilia ndoto zao zinazo watenga na Haki, na zinazo wapotosha.

Na ndani ya Sura hii umebainishwa uhalali wa vyakula alivyo halalisha Mwenyezi Mungu Mtukufu, na upotovu wa Washirikina walivyo jiharimishia wenyewe bila ya kutegemea dalili yoyote, na vipi wanavyo mnasibishia kuharimisha huko Mwenyezi Mungu Aliye Takasika.

Na ndani yake yamebainishwa mambo haya, ambayo ndio mukhtasari wa Uislamu na tabia njema za kusifika. Mambo yenyewe ni:- kuharimisha ushirikina, uzinzi, kuuwa mtu, kula mali ya yatima, waajibu wa kutimiza vipimo na mizani, kutimiza uadilifu, kutekeleza ahadi, kuwatendea wema wazazi, na kukataza kuwazika watoto wa kike nao wahai.

 

KWA JINA LA MWENYEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License