Acts
Chapter 1
1 Ndugu
Theofilo, Katika kitabu cha kwanza niliandika juu ya mambo yote Yesu aliyotenda
na kufundisha tangu mwanzo wa kazi yake
2 mpaka
siku ile alipochukuliwa mbinguni. Kabla ya kuchukuliwa mbinguni aliwapa maagizo
kwa njia ya Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua.
3 Kwa muda
wa siku arobaini baada ya kifo chake aliwatokea mara nyingi kwa namna ambazo
zilithibitisha kabisa kwamba alikuwa hai. Walimwona, naye aliongea nao juu ya
ufalme wa Mungu.
4 Wakati
walipokutana pamoja aliwaamuru hivi: "Msiondoke Yerusalemu, bali ngojeeni
ile zawadi aliyoahidi Baba, zawadi ambayo mlikwisha nisikia nikiongea juu yake.
5 Kwani
Yohane alibatiza kwa maji, lakini baada ya siku chache, ninyi mtabatizwa kwa
Roho Mtakatifu."
6 Basi,
mitume walipokutana pamoja na Yesu, walimwuliza, "Je Bwana, wakati huu
ndipo utakaporudisha ule ufalme kwa Israeli?"
7 Lakini
Yesu akawaambia, "Nyakati na majira ya mambo hayo viko chini ya mamlaka ya
Baba yangu, wala si shauri lenu kujua yatakuwa lini.
8 Lakini
wakati Roho Mtakatifu atakapowashukieni ninyi, mtajazwa nguvu na mtakuwa mashahidi
wangu katika Yerusalemu, katika nchi yote ya Yudea na Samaria, na hata miisho ya dunia."
9 Baada ya
kusema hayo, wote wakiwa wanamtazama, alichukuliwa mbinguni; wingu likamficha
wasimwone tena.
10
Walipokuwa bado wanatazama juu angani, akiwa anakwenda zake, mara watu wawili
waliokuwa wamevaa nguo nyeupe walisimama karibu nao,
11
wakasema, "Enyi wananchi wa Galilaya! Mbona mnasimama mkitazama angani?
Yesu huyu ambaye amechukuliwa kutoka kwenu kwenda mbinguni atakuja tena namna
hiyohiyo mliivyomwona akienda mbinguni."
12 Kisha
mitume wakarudi Yerusalemu kutoka mlima wa Mizeituni ulioko karibu kilomita
moja kutoka mjini.
13
Walipofika mjini waliingia katika chumba ghorofani ambamo walikuwa wanakaa; nao
walikuwa Petro, Yohane, Yakobo, Andrea, Filipo na Thoma, Bartholomayo na
Mathayo, Yakobo mwana wa Alfayo, Simoni Zelote na Yuda mwana wa Yakobo.
14 Hawa
wote walikusanyika pamoja kusali, pamoja na wanawake kadha wa kadha, na Maria
mama yake Yesu, na ndugu zake.
15 Siku
chache baadaye, kulikuwa na mkutano wa waumini, karibu watu mia moja na
ishirini. Petro alisimama mbele yao,
16
akasema, "Ndugu zangu, ilikuwa lazima ile sehemu ya Maandiko Matakatifu
itimie, sehemu ambayo Roho Mtakatifu, kwa maneno ya Daudi, alibashiri habari za
Yuda ambaye aliwaongoza wale waliomtia Yesu nguvuni.
17 Yuda
alikuwa mmoja wa kikundi chetu maana alichaguliwa ashiriki huduma yetu.
18
"Mnajua kwamba yeye alinunua shamba kwa zile fedha alizopata kutokana na
kitendo chake kiovu. Akaanguka chini, akapasuka na matumbo yake yakamwagika
nje.
19 Kila
mtu katika Yerusalemu alisikia habari za tukio hilo na hivyo, kwa lugha yao,
wakaliita lile shamba `Hekeli Dama`, maana yake, `Shamba la Damu.`)
20 Basi,
imeandikwa katika kitabu cha Zaburi: `Nyumba yake ibaki mahame; mtu yeyote
asiishi ndani yake.` Tena imeandikwa: `Mtu mwingine achukue nafasi yake katika
huduma hiyo.`
21 Kwa
hiyo, ni lazima mtu mwingine ajiunge nasi kama shahidi wa ufufuo wake Bwana
Yesu. Anapaswa kuwa mmoja wa wale waliokuwa katika kundi letu wakati wote Bwana
alipokuwa anasafiri pamoja nasi, tangu wakati Yohane alipokuwa anabatiza mpaka
siku ile Yesu alipochukuliwa kutoka kwetu kwenda mbinguni."
22 []
23 Basi,
wakataja majina ya watu wawili; wa kwanza Yosefu aliyeitwa Barsaba (au pia
Yusto), na wa pili Mathia.
24 Kisha
wakasali: "Bwana, wewe unajua mioyo ya watu wote. Hivyo, utuonyeshe ni
yupi kati ya hawa wawili uliyemchagua
25 ili
achukue nafasi hii ya huduma ya kitume aliyoacha Yuda akaenda mahali pake mwenyewe."
26 Hapo,
wakapiga kura; kura ikampata Mathia, naye akaongezwa katika idadi ya wale
mitume wengine kumi na mmoja.
|