Chapter 11
1 Laiti
mngenivumilia kidogo, hata kama mimi ni mjinga kiasi fulani! Naam, nivumilieni
kidogo.
2 Ninawaoneeni
wivu lakini ni wivu wa Mungu; maana ninyi ni kama bikira safi niliyemposa kwa
mwanamume mmoja tu ambaye ndiye Kristo.
3 Lakini
naogopa kwamba, kama vile yule nyoka kwa hila zake za uongo alimdanganya Hawa,
fikira zenu zaweza kupotoshwa, mkauacha uaminifu wenu wa kweli kwa Kristo.
4 Maana
mtu yeyote ajaye na kumhubiri Yesu aliye tofauti na yule tuliyemhubiri, ninyi
mwampokea kwa mikono miwili; au mnakubali roho au habari njema tofauti kabisa
na ile mliyopokea kutoka kwetu!
5 Sidhani
kwamba mimi ni mdogo kuliko hao "mitume wakuu."
6 Labda
sina ufasaha wa lugha, lakini elimu ninayo; jambo hili tumelionyesha wazi
kwenu, kila mahali na kila wakati.
7 Mimi
niliihubiri kwenu Habari Njema ya Mungu bila kudai mshahara; nilijinyenyekeza
ili nipate kuwakweza ninyi. Je, nilifanya vibaya?
8
Nilipofanya kazi kati yenu, mahitaji yangu yaligharimiwa na makanisa mengine.
Kwa namna moja au nyingine niliwapokonya wao mali yao nipate kuwatumikia ninyi.
9
Nilipokuwa nanyi sikumsumbua mtu yeyote nilipohitaji fedha; ndugu waliotoka
Makedonia waliniletea kila kitu nilichohitaji. Nilikuwa mwangalifu sana nisiwe
mzigo kwa namna yoyote ile, na nitaendelea kufanya hivyo.
10 Naahidi
kwa ule ukweli wa Kristo ulio ndani yangu, kwamba hakuna kitakachoweza kunizuia
kujivunia jambo hilo popote katika Akaya.
11 Kwa
nini nasema hivyo? Kwa sababu eti siwapendi ninyi? Mungu anajua kwamba
nawapenda!
12
Nitaendelea kufanya kama ninavyofanya sasa, ili nisiwape nafasi wale
wanaotafuta nafasi, nafasi ya kujivuna kwamba eti wanafanya kazi kama sisi.
13 Maana,
hao ni mitume wa uongo, wafanyakazi wadanganyifu wanojisingizia kuwa mitume wa
Kristo.
14 Wala si
ajabu, maana hata Shetani mwenyewe hujisingizia kuwa malaika wa mwanga!
15 Kwa
hiyo si jambo la kushangaza ikiwa na hao watumishi wake wanajisingizia kuwa
watumishi wa haki. Mwisho wao watapata kile wanachostahili kufuatana na matendo
yao.
16 Tena
nasema: Mtu asinifikirie kuwa mpumbavu. Lakini kama mkifikiri hivyo, basi,
nichukueni kama mpumbavu ili nami nipate kuwa na cha kujivunia angaa kidogo.
17
Ninachosema sasa si kile alichoniagiza Bwana; kuhusu jambo hili la kujivuna,
nasema tu kama mtu mpumbavu.
18 Maadam
wengi hujivuna kwa sababu za kidunia, nami pia nitajivuna.
19 Ninyi
ni wenye busara, ndiyo maana hata mnawavumilia wapumbavu!
20
Mnamvumilia hata mtu anayewafanya ninyi watumwa, mtu mwenye kuwanyonya, mwenye
kuwakandamiza, mwenye kuwadharau na kuwapiga usoni!
21 Kwa
aibu nakubali kwamba sisi tulikuwa dhaifu. Iwe iwavyo, lakini kama kuna mtu
yeyote anayethubutu kujivunia kitu - nasema kama mtu mpumbavu - mimi nathubutu
pia.
22 Je, wao
ni Waebrania? Hata mimi. Je, wao ni Waisraeli? Hata mimi. Wao ni wazawa wa
Abrahamu? Hata mimi.
23 Wao ni
watumishi wa Kristo? Hata mimi - nanena hayo kiwazimu - ni mtumishi wa Kristo
zaidi kuliko wao. Mimi nimefanya kazi ngumu zaidi, nimekaa gerezani mara nyingi
zaidi, nimepigwa mara nyingi zaidi na nimekaribia kifo mara nyingi.
24 Mara
tano nilichapwa vile viboko thelathini na tisa vya Wayahudi.
25
Nilipigwa viboko mara tatu, nilipigwa mawe mara moja; mara tatu nilivunjikiwa
meli baharini, na humo nikakesha usiku kucha na kushinda mchana kutwa.
26 Kila mara
safarini nimekabiliwa na hatari za mafuriko ya mito, na hatari za wanyama;
hatari kutoka kwa wananchi wenzangu na kutoka kwa watu wa mataifa mengine;
hatari za mjini, hatari za porini, hatari za baharini, hatari kutoka kwa ndugu
wa uongo
27
Nimefanya kazi na kutaabika, nimekesha bila usingizi mara nyingi; nimekuwa na
njaa na kiu; mara nyingi nimefunga na kukaa katika baridi bila nguo.
28 Na,
licha ya mengine mengi, kila siku nakabiliwa na shughuli za makanisa yote.
29 Kama
mtu yeyote ni dhaifu, nami pia ni dhaifu; mtu yeyote akikwazwa, nami pia huwa
na wasiwasi. ic
30
Ikinilazimu kujivuna, basi, nitajivunia udhaifu wangu.
31 Mungu
na Baba wa Bwana Yesu - jina lake litukuzwe milele - yeye anajua kwamba sisemi
uongo.
32
Nilipokuwa Damasko, mkuu wa mkoa, aliyekuwa chini ya mfalme Areta, alikuwa
akiulinda mji wa Damasko ili apate kunikamata.
33 Lakini,
ndani ya kapu kubwa, niliteremshwa nje kupitia katika nafasi ukutani,
nikachopoka mikononi mwake.
|