Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Swahili New Testament

IntraText CT - Text

  • Matthew
    • Yesu anawalaumu walimu wa Sheria na Mafarisayo
Previous - Next

Click here to show the links to concordance

     Yesu anawalaumu walimu wa Sheria na Mafarisayo
\r
\is (Marko 12:38-39; Luka 11:43,46; 20:45-46)
\ie

1 Kisha Yesu akauambia umati wa watu pamoja na wanafunzi wake,
2 "Walimu wa Sheria na Mafarisayo wana mamlaka ya kufafanua Sheria
ya Mose.
3 Kwa hiyo shikeni na kutekeleza chochote watakachowaambieni. Lakini
msiyaige matendo yao, maana hawatekelezi yale wanayoyahubiri.
4 Hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani, lakini wao
wenyewe hawataki kunyosha hata kidole wapate kuibeba.
5 Wao hufanya matendo yao yote ili watu wawaone. Huvaa tepe zenye
maandishi ya Sheria juu ya panda la uso na mikononi na hupanua pindo za
makoti yao.
6 Hupenda nafasi za heshima katika karamu na viti vya heshima katika
masunagogi.
7 Hupenda kusalimiwa kwa heshima sokoni na kupendelea kuitwa na
watu: <Mwalimu.>
8 Lakini ninyi msiitwe kamwe <Mwalimu,> maana mwalimu wenu ni mmoja
tu, nanyi nyote ni ndugu.
9 Wala msimwite mtu yeyote <Baba> hapa duniani, maana Baba yenu ni
mmoja tu aliye mbinguni.
10 Wala msiitwe <Viongozi,> maana kiongozi wenu ni mmoja tu, ndiye
Kristo.

11 Aliye mkubwa miongoni mwenu ni lazima awe mtumishi wenu.
12 Anayejikweza atashushwa, na anayejishusha atakwezwa.

     Yesu analaumu unafiki
\r
\is (Marko 12:40; Luka 11:39-42,44,52; 20:47)
\ie

13 "Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnaufunga
mlango wa Ufalme wa mbinguni mbele ya macho ya watu. Ninyi wenyewe
hamwingii ndani, wala hamwaruhusu wanaotaka kuingia waingie.*fj*
\fm j
\fr 23:13
\f
\is Baadhi ya makala zina aya ya 14:
\ie Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnawanyonya
wajane na kujisingizia kuwa watu wema kwa kusali sala ndefu. Kwa sababu
hiyo mtapata adhabu kali.
\is (taz. Marko 12:40)
\ie

14 missing
15 "Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafiri
baharini na nchi kavu ili kumpata mtu mmoja afuate dini yenu.
Mnapompata, mnamfanya astahili maradufu kwenda katika moto wa Jehanamu
kuliko ninyi wenyewe.

16 "Ole wenu viongozi vipofu! Ninyi mwasema ati mtu akiapa kwa
Hekalu, kiapo hicho si kitu; lakini akiapa kwa dhahabu ya Hekalu, kiapo
hicho kinamshika.
17 Enyi vipofu wapumbavu! Kipi kilicho cha maana zaidi: dhahabu au
Hekalu linalofanya hiyo dhahabu kuwa takatifu?
18 Tena mwasema ati mtu akiapa kwa madhabahu si kitu; lakini akiapa
kwa zawadi iliyowekwa juu ya madhabahu, kiapo hicho humshika.
19 Enyi vipofu! Ni kipi kilicho cha maana zaidi: ile zawadi, au
madhabahu ambayo hufanya hiyo zawadi kuwa takatifu?
20 Anayeapa kwa madhabahu ameapa kwa hiyo madhabahu, na kwa chochote
kilichowekwa juu yake.
21 Na anayeapa kwa Hekalu ameapa kwa hilo Hekalu na pia kwa yule
akaaye ndani yake.
22 Na anayeapa kwa mbingu ameapa kwa kiti cha enzi cha Mungu, na kwa
huyo aketiye juu yake.
23 Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnatoza watu
zaka, hata juu ya majani yenye harufu nzuri, bizari na jira, na huku
mnaacha mambo muhimu ya Sheria kama vile haki, huruma na imani. Haya
ndiyo hasa mliyopaswa kuyazingatia bila kusahau yale mengine.
24 Viongozi vipofu! Mnatoa nzi katika kinywaji, lakini mnameza
ngamia!
\il 5
ic
\is Jira (Mat. 23:23)
\ie

25 "Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnasafisha
kikombe na bakuli kwa nje, lakini ndani mnaacha kumejaa vitu mlivyopata
kwa unyang'anyi na uchoyo.
26 Mfarisayo kipofu! Kisafishe kikombe ndani kwanza na nje kutakuwa
safi pia.

27 "Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mko kama
makaburi yaliyopakwa chokaa ambayo kwa nje yanaonekana kuwa mazuri,
lakini ndani yamejaa mifupa ya maiti na kila namna ya uchafu.
28 Hali kadhalika ninyi mnaonekana na watu kwa nje kuwa wema, lakini
kwa ndani mmejaa unafiki na uovu.

     Adhabu inakuja
\r
\is (Luka 11:47-51)
\ie

29 "Ole wenu walimu wa Sheria na Mafarisayo, wanafiki! Mnajenga
makaburi ya manabii na kuyapamba makaburi ya watu wema.
30 Mwasema: <Kama sisi tungaliishi nyakati za wazee wetu
hatungalishirikiana nao katika mauaji ya manabii!>
31 Hivyo mnathibitisha ninyi wenyewe kwamba ninyi ni watoto wa watu
waliowaua manabii.
32 Haya, kamilisheni ile kazi wazee wenu waliyoianza!
33 Enyi kizazi cha nyoka wenye sumu! Mnawezaje kuiepa hukumu ya moto
wa Jehanamu?
34 Ndiyo maana mimi ninawapelekea ninyi manabii, watu wenye hekima
na walimu; mtawaua na kuwasulubisha baadhi yao, na wengine mtawapiga
viboko katika masunagogi yenu na kuwasaka katika kila mji.
35 Hivyo lawama yote itawapateni kwa ajili ya damu yote ya watu wema
iliyomwagwa juu ya ardhi. Naam, tangu kuuawa kwa Abeli ambaye hakuwa na
hatia, mpaka kuuawa kwa Zakariya, mwana wa Barakia, ambaye mlimuua
Hekaluni kati ya patakatifu na madhabahu.
36 Nawaambieni kweli, kizazi hiki kitapata adhabu kwa sababu ya
mambo haya.

     Jinsi Yesu alivyoupenda mji wa Yerusalemu
\r
\is (Luka 13:34-35)
\ie

37 "Yerusalemu, Ee Yerusalemu! Unawaua manabii na kuwapiga mawe
wale waliotumwa kwako. Mara ngapi nimejaribu kuwakusanya watoto wako
kwangu, kama vile kuku anavyokusanya vifaranga vyake chini ya mabawa
yake, lakini hukutaka.
38 Haya basi, nyumba yako itaachwa mahame.
39 Nakwambia kweli, hutaniona tena mpaka wakati utakaposema:
  <Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Bwana.">
\il 5
ic
\is Kuku na vifaranga vyake (Mat. 23:37)
\ie
\fr 23:39
\f Taz Zab 118:26

 




Previous - Next

Table of Contents | Words: Alphabetical - Frequency - Inverse - Length - Statistics | Help | IntraText Library

Best viewed with any browser at 800x600 or 768x1024 on Tablet PC
IntraText® (V89) - Some rights reserved by EuloTech SRL - 1996-2007. Content in this page is licensed under a Creative Commons License